Monday 10 September 2007

Tuanzie wapi...Things Do NOT Just Happen

Ndio, vitu haviwi tu hivihivi, tuanzie wapi, maana mpaka sasa hatujui tuko wapi na nina shaka kama bado tunakumbuka tulikotoka. kila siku maneno ya kupongeza maendeleo HEWA yanarushwa redioni, kwenye televisheni na kwenye mabango makubwa kuliko nyumba zilizokaribu na mabango hayo.

Tazama picha hapo juu halafu unambie kama walijenga tuu bila PLAN, kama hakuna mfumo maalumu wa kuhakikisha elimu, ubunifu unatumiwa katika miradi ya kuleta maendeleo hakuna kitakachokua, ndio maana kila siku utasikia mtaa fulani nyumba zitavunjwa kupisha ujenzi wa barabara, matokeo yake ni kupoteza pesa za taifa katika kulipa fidia kitendo ambacho kingeepukwa kama kungekuwa na mfumo wa kusimamia ujenzi mijini na mahala popote pale. watu wanajijengea kiholela kwasababu hakuna mipango ya ujenzi miji ndio maana nyumba zimeshikana kama matundu ya ndege hakuna njia ya kupita gari ama maeneo wazi.. ikitokea hatari msaada hauwezi fika kwa wakati.

HIVI MAOFISA KWENYE WIZARA YA ARDHI WANAFANYA KAZI GANI, MIAKA AROBAINI NA SITA LAKINI SIJAONA LA MAANA WANALOFANYA KUDHIBITI UJENGAJI KIHOLELA, NA SILAUMU WAJENGAJI KWASABABU HAKUNA MAELEKEZO TOKA KWA WAHUSIKA, UKISHA MALIZA KUJENGA KIBANDA CHAKO WAO WATAJIFANYA WATAALAMU WA KUJA KUBOMOA ILI WAKURUDISHE KWENYE UMASIKINI WAKATI TAYARI ULISHAANZA KUJIKOMBOA.

PITA MITAA AMBAYO TAYARI BARABARA ZIMEKARABATIWA NA KUWEKWA LAMI, UTAKUTA JAMAA WENGINE WANAKUJA KUCHIMBA MAHANDAKI WAKIMALIZA KAZI YAO WANAYAACHA WAZI AMA WANAWEKA KIFUSI, BADALA YA KUREKEBISHA KAMA WALIVYOKUTA...MWISHO MMOMONYOKO UNAHARIBU BARABARA NZIMA..WAHUSIKA WAKO WAPI..NANI ANAPASWA KUFUATILIA UTUNZAJI WA BARABARA?

WENZETU WALIO KWENYE NCHI ZILIZOENDELEA WAMEWEKA TARATIBU AMBAZO LAZIMA ZIFUATWE, NA PIA WASIMAMIAJI WA KUHAKIKISHA TARATIBU HIZO ZINAFATWA tena BILA RUSHWA , KATIKA KILA JAMBO KUANZIA UJENZI WA BARABARA, NYUMBA, HOSPITALI, MASHULE, MAHOTELI NA KILA KITU ILI KUHAKIKISHA UBORA WA MAISHA UNALINDWA NA KUENDELEZWA.

SISI RUSHWA NDIO MTENGEZAJI WA YOTE UNAWEZA KUPINDA CHOCHOTE ILI MRADI UNA PESA ZA KUHONGA..NAFIKIRI MUDA WA KUENDEKEZA MATUMBO UMEKWISHA SASA TUANZE KUJENGA MAENDELEO YA KWELI KWA KUONDOSHA KILA AINA YA UPENYO WA MIANYA YA RUSHWA PIA KUWEKA TARATIBU MAALUM KUSIMAMIA KILA KITU NA PIA KUWEKA WAZI TARATIBU HIZO ILI KILA MTU AJUE HAKI YAKE NA IWE RAHISI KUPATIKA KWA HAKI HIYO BILA YA VIKWAZO VYA UKIRITIMBA.

TUANZIE KWENYE ELIMU MAANA NDIO MAMA WA YOTE..MATATIZO TULIYONAYO NI KWASABABU YA UKOSEFU WA ELIMU BORA..NA NINAMAANISHA ELIMU BORA SIO HII TULIORITHI KWA WAKOLONI..


No comments: