Friday 7 September 2007

Upumbavu wa Mwafrika...Mbele ya Mzungu









Mniite Mbaguzi, lakini kwa hili lazima niseme, SHIDA ZOTE ZILIZOPO AFRIKA HII LEO ZIMELETWA NA WAZUNGU KWA NJIA MOJA AMA NYENGINE NA YOTE HII NI KWA AJILI YA KUJINUFAISHA WAO. Hivi niwaulize jamani huu utalii wa kuja na kuua wanyama katika mbuga zetu una faida gani je thamani ya maisha ya wanyama hawa ni pesa chache zinazochapishwa na hao hao wazungu, WANAKUJA na bunduki zao wakijifanya ni wawindaji, halafu na sisi kwa upumbavu wetu na kukosa akili tupo mbele kuwaongoza katika kuangamiza maliasili zetu, mbona kwao ukiuwa paka utalaaniwa na kila chombo cha habari kwamba wewe ni shetani hufai kuishi pamoja nao sasa leo iweje watoke kwao na kuja kwetu kwa kisingizio cha utalii ambacho tafsiri yake haina uhusiano na mauaji ya wanyama pori wasio na hatia. hawa si watalii bali ni waangamizaji wanaopenda kumwaga damu za viumbe bila sababu za msingi. TROPHY hunting ni upumbavu kwa binadamu mwenye akili timamu, nani kama si mwendawazimu anayependa kuona kichwa cha simba kilichotundikwa kwenye ukuta wa sebule anamoishi maana kama ni uhodari na ujasiri kwanini watumie bunduki kuua.
UTAJIRI ASILIA UMEKUWA LAANA JUU YETU, HATUNA UTAMADUNI WA KUTHAMANISHA MALI ZETU LAU KAMA INGEKUWA WANYAMA HAWA WAKO NCHI ZA ULAYA HAKUNA AMBAYE ANGETHUBUTU KUUA, LEO HII NCHI KAMA YA UINGEREZA, HUWEZI KWENDA PORINI KUTAZAMA MWEWE KAMA HUNA KIBALI CHA KUTAZAMA WANYAMA, SISI WAPUMBAVU TUSIO NA AKILI NA MAARIFA TUNAWATANGAZIA KUWA NJOONI MUUWE SIMBA, NYATI, TEMBO, CHUI ILI MRADI MTUPE PESA. PESA KITU GANI KAMA MASHINE ZAO ZA KUCHAPISHA HAZIJAWAHI KUZIMWA TOKA ZIANZE KUFANYA KAZI, WANATUMIA HAYO MAKARATASI KUCHUKUA MALI, NIPE DHAHABU NIKUPE MAKARATASI, NIPE ALMASI NIKUPE MAKARATASI, NIPE ARDHI NIKUPE MAKARATASI, NATAKA KUUA SIMBA KUMI NITAKUPA MAKARATASI....MAKARATASI YAKO HAYANA THAMANI YANGU TU NDIO YENYE THAMANI...KARATASI LANGU MOJA SAWA NA YAKO ELFU NA MIA MOJA....UPUUZI MTUPU.
HIVI KWANI MAENDELEO NI MPAKA TUWE KAMA WAZUNGU, TUVAE, TULE, TULALE, NA PIA RANGI ZA NGOZI ZETU ZIWE KAMA ZAO MAANA ZA KWETU TUNAONA HAZINA THAMANI, INABIDI TUJICHUBUE...
UWINDAJI NA UUWAJI WA WANYAMA KWA JINA LA UTALII UKOMESHWE KWA AJILI YA KIZAZI HIKI NA VIZAZI VIJAVYO...
HAWA JAMAA WAMEPOTEZA NA KUTOKOMEZA AINA NYINGI ZA WANYAMA KUTOKANA NA USHETANI WAO.. NA SISI JINSI TUNAVYOWASAIDIA TUTAKUWA KAMA WAO WANYAMA WATATOWEKA, TUBAKI PATUPU.






2 comments:

Awadh said...

na kubalian na wewe mia kwa mia matatizo Africa ya natoka injee na pesa hizo wanazoleta, kesho sisi ndiyo tutalia.lazima watu wa zidi kuilimishwa.

Anonymous said...

hata mimi nakubaliana nawe kabisa