Tuesday 17 May 2011

Ni lini serikali za Afrika zitatumia wasomi katika Maamuzi

Imekuwa ni desturi kwa serikali za nchi nyingi za Afrika kufanya maamuzi makubwa yahusuyo Uchumi,Afya,na maendeleo Jamii kisiasa. Kama nikikumbuka vyema Siasa ni muhimu katika jamii lakini mchango wake lazima uwe unategemea Elimu iliyothibitika. Katika dunia ya sasa ya Utandawazi ama globalisation nchi isiyofanya jitihada maalumu za kujikwamua kwa kutumia michango ya elimu mbali mbali ambazo zimo ndani na nje ya nchi zitajikuta zikiyumba na mwisho wake amani na imani waliyonayo wananchi itatoweka pia.

Nchi za Magharibi zinafanya kila jitihada kuhakikisha wananchi wake wanapata mahitaji yao ya msingi kwa gharama nafuu na kwa ubora wa hali ya juu..cha kusikitisha nchi nyingi za kiafrika ikiwemo Tanzania zimejivua jukumu hilo na kuwa na kila mtu ale kwa urefu wa mikono yake ama Hands-off approach. Majukwaani wanahubiri ya Musa vitendoni wanatenda ya Firauni.

Mambo muhimu kama uboreshaji wa huduma za afya na elimu zinasubiri wahisani na misaada yao wakati kodi inatumika kulipa mishahara na marupurupu ya waendeshaji serikali wakiwemo wabunge ambayo iko juu zaidi ya mawingu tena bila woga wala haya juu ya wananchi wenziwao ambao ni masikini hata kujua watakula nini kesho ni ukuta.

Itakuwa sawa kwamba wasomi ni adui wakubwa wa serikali za kiafrika ndio maana wengi wao wamekimbia nchi zao na kunufaisha nchi za magharibi na kwengineko.Rafiki yangu mmoja alinambia hatutaki wasomi bakini huko huko. Ukiwa na mwerevu katika kundi la wajinga basi wewe ndio utakuwa mjinga na wao ndio werevu kwasababu wingi ni nguvu hata kama ni ujinga.

No comments: