Thursday 19 May 2011

Ulafi wa Viongozi wa Nchi Afrika na Hand-off Approach



Nchi nyingi za Afrika ziko mikononi mwa serikali ambazo zinaongozwa na watu wasio na chembe ya huruma kwa umma wanaoongoza. Wengi wao ni urithi tulioachiwa na wakoloni kwa hiyo dhamira zao hazijabadilika toka kuwa watumishi wa kikoloni kunyonya wananchi wenzao mpaka wakawa wenye uchungu na nchi na kujivika taji la uzalendo.






Uzalendo ni kitu adimu katika serikali hizi japo majukwaani huhubiri uzalendo utadhani uzalendo ni nguo unayoweza kuifua na kuivaa. Uzalendo uko moyoni, uzalendo ni sumu ya unyonyaji, uzalendo ni sumu ya rushwa, uzalendo ni sumu ya ukandamizaji, uzalendo ni sumu ya uonevu, uzalendo ni dawa kwa wananchi.



Uzalendo ni chachu ya ukombozi na uzalendo ni chocheo ya maendeleo ya nchi
Uzalendo huleta upendo katika nchi huleta neema huleta amani huleta furaha ya nchi
.


Leo hii viongozi wameamua kujivua majukumu ya kuhakikisha wananchi wanapata fursa sawa katika kushiriki masuala ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Eti ni jukumu la wananchi kuleta maendeleo wakati wao wanazidisha kujenga vipingamizi vya maendeleo hayo. Mwananchi akifanya biashara badala ya kusaidiwa kielimu na kifedha ili aweze kuendelea, itafanywa kila mbinu ili asifikie lengo na mwisho kukata tamaa.






Pesa za kodi zinaishia kujenga mahekalu na kununua magari ya kifahari ya viongozi wakati wananchi nyumba zao za udongo zilizoezekwa nyasi. Shule hazina viti vya kukalia wala walimu wa kutosha, hospitali hakuna vitanda wagonjwa wanalala chini na hakuna dawa za kutosha wala madaktari wa kutoa huduma..Eti kiongozi mzima anasema nendeni LOLIONDO MTAPONA!!!!

No comments: